MATATIZO YA KURITHI YANAVYOWEZA KUATHIRI UCHUMI WAKO.


Mwanzo 12:10-11
Kurithi ni nini?.  Kurithi  ni kupokea kitu kutoka mikononi mwa mtu mwingine ambacho  kilikuwa  ni  mali yake  mwenyewe na kumrithisha mtu mwingine.   

MFANO:
Kupokea shamba ,Nyumba, Gari, Baiskeli n,k  kutoka kwa mzazi wako/ mlezi wako na kukupa wewe au mtu mwingine ambavyo tangu awali vilikuwa ni vya kwake yaani mali yake mwenyewe anaamua kumpa/ kumkabithi mtu mwingine urithi wake.
·        IBRAHIMU alizaliwa na mzee Tera,baada ya gharika ya NUHU,na baada ya kuzaliwa walikuwa wanaishi sehemu nmoja iitwayo URU WA WAKALDAYO.
·        Wakatoka uko wakaenda kaanani wakafika mpaka wa HARANI wakakaa huko.
·        BWANA alipomtokea IBRAHIMU  alimwambia atoke  katika nchi ile aende KAANANI  na alipofika  KAANANI  alitembelea  katika miji kadha wa kadha  lakini mwisho wa siku nchi ile ikaja kukumbwa na njaa .
·        IBRAHIMU  akaamua kwenda uko MISRI  kwa ajili ya kutafuta chakula ale asije kufa kwa njaaa

                                                            IBRAHIMU.
1.     Alikumbwa na njaa katika nchi ya  KAANANI akakimbilia MISRI.
2.     Alikuwa ni mwongo kwa ajili ya hofu.

Ø Alipoenda MISRI  alimwambia mke wake kuwa  Wamisri  wakikuuliza sema wewe ni dadangu  kwakuwa wewe ni mzuri sana wa uso wasije wakaniua mimi wakakuacha wewe uishi hai.

Ø Hapa tunaona kwamba WIVU  mtu unayempenda  lazima utamuonea sana wivu kila wakati,Lakini sasa wa IBRAHIMU ulipitiliza.
Ø IBRAHIMU  alipoenda nchi ya kusini kwa wafilisti alidnganya vile vile kwa hofu ile ile ya kuwa Yule sio  mke wake bali ni dada yake.

v ABIMELEKI  mfalme wa GERARI  akatuma watu waende kumposaa
v Lakini kwakuwa ABIMELEKI   Mfalme wa GERARI alikuwa ni mtu  mkamilifu mbele za BWANA, alikuwa akitenda mema na haki, mbele za BWANA, ndipo BWANA akamuonya katika ndoto  kuwa asitende dhambi Yule ni mke wa mtu.

ü Tuwe wakamilifu mbele za BWANA ili BWANA  atuokoe tusitende dhambi bila ya kujua.
ü Tukiwa wakamilifu mbele za BWANA atautpigania sisi na wana wetu.

                                      MATATIZO KADHAA YA KURITHI.
1.     IBRAHIMU  mke  wake  alikuwa ni tasa.Yaani  SARA
2.     IBRAHIMU  yeye  alikuwa ni mwongo na muoga anadanganya huyu sio mke wangu ni ndugu yangu ili asije akauwawa.
3.     IBRAHIMU  alipatwa na Njaa 12:10.
4.     ISAKA  mke wake naye alikuwa ni tasa kama Baba yake  25:21 .
5.     NJAA  Isaka  naye alipitia kipindi kigumu kama cha BABA yake  katika nchi yao wenyewe  walipokuwa wanaishi nchi ya GERARI.
6.     ISAKA  akadanganya  kama  BABA yake  kwamba REBEKA  ni ndugu yake  katika nchi ya GERARI. 26:6

ü Matatizo hayo ya kurithi yaliendelea kwenye familia ya mzee IBRAHIMU   hadi kwa mjukuu wake Yakobo.
ü Yakobo alioa wake wawili mkubwa ni  RAHELI  na  Mdogo ni LEA .
ü LEA alikuwa  tasa  hazai  lakini  RAHELI  alikuwa na watoto.

7.     ROHO za chuki kuchukiana na hiyo ilianzia kwa SARA  na HAJIRI  wake za IBRAHIMU  mpaka  kwa wake za YAKOBO na watoto wao.

Ø Yusufu alipokuwa akichunga kondoo na ndugu zaake  wana wa BILHA  na ZILPA   Vijakazi wa  LEA  na RAHELI   walimchukia saana YUSUFU .
Ø Walimchukia  sana YUSUFU  Kiasi kwamba wakaazimia kumuua ili maono yake na ndoto zake zisitimie.
Ø Lakini piaa waliposhindwaa wakaamua kumuuza ndugu yao  kwa  vipande 20 vya fedha na kusingizia ameraluriwa na mnyama mkali .

                                                      YAKOBO.
1)     Alikuwa ni mjukuu wa IBRAHIMU , alipitia katika kipindi kigumu sana kama cha BABU yake na BABA yake  ya NJAA na UTASA.
2)    Mke wake  YAKOBO alikuwa   tasa hazai ,
3)    YAKOBO  alipatwa na njaa kubwa  katika taifa lao la KAANANI walilokuwa wanaishi wenyewe , kaama BABU yake na BABA yake walivyopatwa na njaa.


Wakati mwingine sisi kama wanadamu tunapitia katika wakati mgumu sana wa maisha bila ya kujua vyanzo vyake vimesababishwa na nini  na kipi  tufanye lkn ni matumaini yangu kuwa leo umejifunza namna ya kuvishughurikia vyanzo vya matatizo yako ya kiuchumi  uliyonayo.


Ni mimi ndugu yenu katika KRISTO YESU 
BARAKA AUDAX
INJILI YA KRISTO ZANZIBAR
+255 717 461006

Comments

Popular Posts