NDOTO UNAZOOTA USIZIDHARAU KWANI ZINAKUWA NA UJUMBE WA MAISHA YAKO

NDOTO UNAZOOTA USIZIDHARAU KWANI ZINA MAANA,NA UJUMBE WA MAISHA YAKO.                   BWANA YESU asifiwe.  



Karibu Leo tunachambua ndoto na maana zake na makusudi yake.                                                                     MUNGU Hutumia Ndoto Kama Sehemu Muhimu Kwake Kusema Na Mwanadamu Ili Kumjulisha Mambo Yaliyokusudiwa Kutoka Sehemu Zifuatazo
  (1) Kutoka Ufalme Wa MUNGU                                                                             (2)Kutoka Ulimwenguni                                                                                                                                                (3) Kutoka Ulimwengu Wa Giza(malango Ya Kuzimu).                             Lengo Kuu La MUNGU Kupitia Ndoto Uliyoota  ni                                                                                
  (1) Kupa Ufahamu Juu Ya Kuenenda Duniani                                                                                                                                                 (2) Kukupa Ramani Ya Safari Yako Duniani.                                                                                                                                                  (3) Kukupa Sehemu Ya Mazungumzo Kati Yako Na Yeye                     (4) Ndoto Ni Njia Pekee Rahisi Ya MUNGU Kukufikia.          - Ndoto Huumba Imani Ya Ushindi,                                                 - Uwe Mwepesi Kutambua Kosa Lako,                                         -Ndoto Hukuhakikishia Ushindi Kama Tu Ukiendelea Na Utakatifu Na Maombi Huku Ukimtii BWANA YESU.                                  Mwanzo 15:1 "Baada Ya Mambo Hayo Neno La BWANA Likamjia Abrahamu Katika Njozi(ndoto), Likinena, Usiogope, Abrahamu, Mimi Ni Ngao Yako , Na Thawabu Yako Kubwa Sana"                                                                                                    Ndoto Nyingine Ni Neno La MUNGU La Moja Kwa Moja Kwako. BWANA YESU Anakupenda Sana.                                           - Ndoto Inapokuja Kwa Kasi Na Nguvu Harafu Kumbukumbu Yake Haipotei, Tena Inakupa Mshituko, Hiyo Inaonyesha Kwamba Majira Ya Tukio Yako Karibu Mno. Kama Jambo Uliloliona Ndotoni Linakutokea Na Vizuri Uchukue Hatua Ya Makusudi Tena Ya Haraka Kama Yeye Alivyokuonyesha Kwa Mshituko.                                     Kama Umeota Shambulio Au Uharibifu Basi Fanya Maamuzi Ya Ghafla Na Sahihi Yenye Kuleta Upenyo Wa Kujibu Hiyo Taarifa, Omba Ndugu Yangu, Mwite BWANA YESU Akuokoe Ili Usiingie Kwenye Uharibifu.                                                                                                                       YESU Alidhihilishwa Ili Azivunje Kazi Za Shetani(1 Yohana 3:8b). Kama Hujaokoka, Ndugu Yangu Hakikisha Unaokoka Leo, BWANA YESU Yuko Kazini Muda Huu Akikutafuta Ili Akuokoe Usiende Motoni Na shetani Naye Yuko Kazini Akitaka Akupeleke Motoni. Ndugu Yangu Ni Heri Kumkimbilia BWANA YESU Leo, Dunia Itapita Na Mambo Yake Lakini Uzima Wa Milele Wa BWANA YESU Ni Wa Milele. Wokovu Ni Leo Wala Sio Kesho. Ndugu Using'ang'anie Dhambi Bali Nga'ng'ania Utakatifu Huku Ukiwa Umeokoka. MUNGU BABA Anakupenda Sana.                      -Mtambo Wa Ndoto Uko Mbinguni Na Wewe Ni Kituo Cha Matangazo Hivyo Kupokea Ndoto Sio Hiari. MUNGU Akitaka Kukupa Ujumbe Anahakikisha Kwamba Viungo Vyako Vyote Vimetulia. MUNGU Anaweza Kuleta Ndoto Kama Sehemu Ya Majibu Ya Maswali Uliyonayo Au Mpango Ulionao.                     Mithali 16:1 "Maandalio Ya Moyo Ni Ya Mwanadamu Bali Jawabu La Ulimi Hutoka Kwa MUNGU".                                 -Ndoto Njema Itatimizwa Kwa Wakati Wake, Ijapochelewa Ingojee.                                                                                   Habakuki 2:2-3 "BWANA Akajibu Akasema Iandike Njozi(ndoto) Ukaifanye Iwe Wazi Sana Katika Vibao, Ili Aisomaye Apate Kuisoma Kama Maji. Maana Njozi(ndoto) Hii Bado Ni Kwa Wakati Ulioamriwa, Inafanya Haraka Ili Kuufikilia Mwisho Wake; Wala Haitasema Uongo; Ijapokawia Ingojee, Kwa Kuwa Haina Budi Kuja, Haitakawia."

 Ndoto Ni Ujumbe Unaojitosheleza. Ndoto Inaeleza Mahali, Nyakati Na Majira Ya Utimilifu Wake. Ndoto Kutoka Kwa MUNGU Haibadiliki Wala Haikosolewi. Kama Unaota Ndoto Inathibitisha Kwamba Ufahamu Wako Haujaharibika. BWANA YESU Anakupenda Sana, Mpokee Leo Utakuwa Umefanya Vyema Sana Sana.                                                                                     -Kwenye Ndoto Pombe Huwakilisha Ibada Ya Sanamu,                          -Mlima Huwakilisha Jaribu Au Viongozi Wakubwa,                  -Bonde Huwakilisha Anguko.                                                         -Mbegu Huwakilisha Neno La MUNGU.                                      -Fimbo HuwakilishaMateso                                                                                                                 Farasi Huwakilisha Safari Au Mbio Au Mwendo.                          -Ukiota Farasi Anakimbia Kwa Spidi Sana Maana Yake Fanya Bidii. Yuko YESU KRISTO Mwenye Uweza, Penye Tatizo Ita Damu Ya YESU, Tii Neno La MUNGU Na Liishi Neno La MUNGU. Omba Bila Kuacha:                                                         Tumia Waefeso 4:12, Mathayo 7:7, 2 Kor 10:5, Kumb 28:1 Yeremia 17:9-10 Wagalatia 5:16 Na Mithali 16:3.                          BWANA YESU Anakupenda Sana Na Hakikisha Unaomba Maombi Ya Vita, Acha Dhambi Na Mtii MUNGU Siku Zote. - Kwenye Ndoto.                                                                                                         - Samaki Huwakilisha Watu,                                                               -Matawi Huwakilisha Uzao,                                                   -Bahari Huwakilisha Watu Wakaapo Au Machafuko,                     -Kisima Huwakilisha Makimbilio,                                                     - Vilima Huwakilisha Vikwazo. Ndugu Yangu Kumwita YESU Kwenye Tatizo Lako Ni Jambo Jema Kuliko Yote, Omba Ndugu Yangu, Omba Maombi Makali Ya Vita Ili Adui Akukimbie,                                                                                     Tumia: Marko 9:23, Yohana 14:14 Ayubu 19:25 Na Mathayo 7:7. Ubarikiwe Sana Na BWANA YESU Anakupenda Sana.                            - Kwenye Ndoto Kondoo Huwakilisha Unyenyekevu Au Utii, -Nzige Huwakilisha Wakati Wa Mema Haujafika,                            -Asali Huwakilisha Yaliyokuwa Machungu Yatakuwa Matamu, -Muhuri Huwakilisha Kuthibitisha Au Hakika Au Yatatimia Au Iwe Siri,                                                                                      -Jangwa Huwakilisha Kipindi Cha Ukame Au Majaribu Au Kipindi Kigumu Kinakuja,                                                                        -Mawimbi Huwakilisha Uharibifu         

-                                        Matunda Huwakilisha Uzao Au Matendo. BWANA YESU Anakupenda Sana Na Hakikisha Unampokea Kuwa BWANA Na MWOKOZI Wa Maisha Yako, Kataa Dhambi, Ogopa Dhambi, Ikimbie Dhambi Na Usifanye Dhambi Na Usifanye Dhambi. Ukiota Ndoto Hakikisha Unaomba Mponde shetani Na Watoto Wake Wote Kwa Jina La YESU KRISTO.                   
Tumia Isaya 54:17, Mathayo 18:18, Waefeso 6:11-12, Yeremia 33:3 Na Mithali 18:10. Ubarikiwe Sana Na BWANA YESU Anakuhitaji Sana Kwenye Ufalme Wake.                                             - Kwenye Ndoto Nguruwe Huwakilisha Umejichafua Wewe, Jitakase,                                                                                         -Malaika Huwakilisha Ujumbe,                                                                     -Baragumu Huwakilisha Mwito,                                                         -Kuoga Maji Huwakilisha Umetakaswa,                                             - kuogelea Baharini Huwakilisha Kucheza Au Kutekwa Na Mambo Ya Kidunia,                                                                              -Miguu Mitupu Huwakilisha Huna Utayari                    -                               Kijani Kibichi Huwakilisha Kustawi,               -Majani Yameota Kwenye Shamba Huwakilisha Uharibifu Umekusudiwa. Yuko Simba Wa Kabila La Yuda YESU KRISTO Mtenda Miujiza, Mwite Na Utakaa Salama, Kataa Kutumika Kwa shetani Na Mkimbilie BWANA YESU. Omba Maombi Makali Na Utakuwa Huru Mbali Mashetani Wote,na kama                                              Hujaokoka Okoka Leo Maana Neema Hiyo Ni Ya  Omba Ukitumia Zaburi 23, Yeremia 1:10-12, Mathayo 5:8,Kameo Yakobo 4:7, Mithali 16:3, Mithali 3:6-7, Na Yohana 15:5b. Sio Kesho. Na Neema Ya Leo Ni Tofauti Na Neema Ya Kesho, Maana Ukiokoka Leo BWANA Atakupa Mme/Mke Sahihi Na Wote Mkiwa Kwenye Wokovu Lakini Ukikataa Kuokoka Leo Unaweza Ukapata Neema Ya Kuokoka Kesho Ila Ukiwa Tayari Na Ukimwi. Ndugu Heri Leo Kuliko Kesho, Hakika BWANA YESU Anakuita Leo.                                               -Kwenye Ndoto Ukiota Giza Mbele Yako Maana Yake Hueleweki Kwa MUNGU,                                                                                   - Daftari Na Kalamu Huwakilisha Matendo Au Mambo Yako Yameandikwa,                                                                                    - Ukijiona Shule Huwakisha MUNGU Mwenyewe Atakufundisha, -Meli Au Boti Au Mtumbwi Huwakilisha Kwamba Mazingira Yanayokuzunguka Ni Ya Uovu,                                            -Mwanga Mbele Yako Huwakilisha Kwamba MUNGU Atakutangulia Au Njia Mbele Yako I Wazi,                          -Nyangumi Au Samaki Mkubwa Huwakilisha Kwamba Mtu Mkubwa Mwovu Atampokea YESU. Ndugu Yangu Kama Hujampokea YESU Muda Wa Kufanya Hivyo Ni Leo Pia Maombi Baada Ya Kuota Ni Muhimu Sana, Omba Ndugu Yangu, Tumia Mistari Hii Kuomba Mathayo 5:6-8, Zaburi 113:3-9 Na Zaburi 27:1-4.                                                                                                   -Kwenye Ndoto Kuvua Samaki Huwakilisha Kuwashuhudia Watu Neno La MUNGU, Wewe Uliyeota Hivyo Changamka Kutumika, -Kubeba Au Kukusanya Samaki Maana Yake Utawahudumia Watakatifu.                                                                              -Ukiona Kwenye Ndoto Samaki Waliooza Maana Yake Watakatifu Wamejiharibu,                                                                                  -Upinde Wa Mvua Huwakilisha MUNGU Amekukumbuka Na Atatimiza Alichokuahidi, Ndugu Maombi Ni Muhimu Kwako, Mwite BWANA YESU Akuponye Na Kukuokoa, Omba Ukitumia Kumb 28:1, Zaburi 60:12, Zaburi 83:18 Na Wafilipi 2:10. -Kwenye Ndoto Ukingo Wa Bahari Au Pwani,                               -Beach Huwakilisha Mapepo/majini Yamekuzunguka, Ndugu Chukua Hatua Za Maombi Kupitia Jina La YESU KRISTO, -Ukiota Bahari Iliyotulia Maana Yake Mambo Yako Shwari Lakini Hayajaondoshwa Hivyo Unatakiwa Kuomba, Omba Ukitumia Ufunuo 12:11, Wagalatia 5:20-22 Na Nahumu 1:9. Ubarikiwe Sana Na Kama Hujaokoka Ndugu Unakosa Uzima Bure, Okoka Ndugu Yangu, BWANA YESU Anakuhitaji Sana. Ubarikiwe Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani ariko KRISTO.


Naamini  utakuwa umebarikiwa  
Ni  mimi  ndugu  yako  
Baraka Audax 
Injili  ya Kristo  Zanzibar.
0717  461006.

Comments

  1. Amen barikiwa sana, na ukiota unatembea barabaran badae unagundua umegeuza nguo unahangaika kutafuta sehemu urekebshe uvae vzur unakosa nn maana yake asante

    ReplyDelete
  2. Amen barikiwa sana, na ukiota unatembea barabaran badae unagundua umegeuza nguo unahangaika kutafuta sehemu urekebshe uvae vzur unakosa nn maana yake asante

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular Posts