JIHADHARI NA MANENO YA WANADAMU.

SOMO:  :     JIHADHALI  NA MANENO  YA    WANADAMU:



Somo  letu  la  leo  tunakwenda  kujifunza  kuhusu  kujihadhari  na  wanadamu:

Unapokuwa  katika  kipindi  kigumu  cha maisha  ambacho  ni  kipindi  cha  mpito  watu  wengi  sana  wanaweza  kukushambulia  kwa  maneno  na  kukusababishia  maumivu  mengi  moyoni.


Ayubu 2:

Hapo  tunaona  kuwa  pamoja  na  kufanikiwa    kimaendeleo  na  uchumi  mzuri  aliokuwa  nao  AYUBU, lakini    bado   shetani  alikuwa  anamuwinda  kwa  nguvu   kwa  kumchongea  sana  mbele  za   Mungu  ila  Mungu    hakumuruhusu. 
Ayubu 2:3(e) Ujapokuwa  ulinichochea  juua  yake, ili nimwangwamize  pasipokuwa  na  sababu.

Ndivo  ilivo  kwa sisi  wana  wa Mungu  kwamba  tunaweza  kuwa  tunapitia  katika  mazingira  magumu  lakini  pamoja  na  hao  kama  Mungu  bado  hajaruhusu  uhangamie  bado  atazidi  kukulinda  tu.

MANENO  YA WANADAMU:

Unapokuwa   unapitia  katika  kipindi  hicho  kigumu  bado  wanadamu   wanazidi  kukuhandama  sana  ila kumbuka  sana  usije  ruhusu  mpenyo  wa  kipepo ukakuharibia  maisha  yako, na  mpenyo  huo  ni kama  kujibizana  nao  vibaya  wanaokutamkia  vibaya  na  kukudharau  saa  nyingine  wanakutukana  kutokana  na kipato  cha  maisha  yako  kilivo   kwa  sasa  ila  naamini  kuwa  Mungu  aliyekuumba  hawezi  kukuacha kabisa uhangamie.
 MFANO:  Ayubu 2:9
Ndipo mkewe  akamwambia, je! Wewe  hata  sasa washikamana  na utimilifu  wako? Ukamkufuru  MUNGU  ukafe.

Hapo  tumeona  mkewe  Ayubu  ndo  anakuwa  wa  kwanza  kumwambia  maneno  ya  maudhi, yawezekana  wanafunzi  wenzako  wakawa  wanakwambia  maneno  ya  maudhi  na  kukudharau  kwa  ajili  ya  kipato  au  kushuka  kwako  darasani napenda  nikwambie  muangalie  Bwana  aliyekuumba  na  mlilie  yeye  peke  yake  wasikushughulishe  hao.

Yawezekana  wapangaji  wenzako  wakakuinukia  na  kukwambia  maneno  yasiyofaa  ya  kejeli  na  maudhi  usiwaangalie  na kuanza  kujibizana  nao  maneno  wala  usimjibu  mpunbavu  sawa  aswa  na  upumbavu  wake  usije  ukafanana  naye.


Siku  moja  nilikuwa  mahali  fulani  nikiwa  nimeharikwa  na  mpendwa  mmoja nyumbani  nikiwa  pamoja  na  watumishi  wenzangu  nikasikia  wanawake  wa  mle  ndani  wakimjadili  mwenzao  aliyekuwa  anapika  dagaa  na  kumtolea  maneno  ya  dhihaka  nyingi  mno. Tumechoshwa  na  harufu  ya  misumari  humu  ndani misumari  yenyewe  inachoma  kabla  haujaila  sasa  ukiiweka  tumboni  itakuwaje.

Nilipowafuata  na  kuwahubiri  injili  ya  BWANA  walitubu  dhambi  zao  na  kujiona  kuwa  walichokuwa  wanafanya  sio  haki  mbele  za  Mungu  ivyo  maneno  ya  wanadamu  wasikusababishe  kukutoa  katika  mpango  wa BWANA  maana  yeye  anajua  mawazo  anayokuwazaia  katika  maisha  yako  ya  baadae'

Hakika  naamini  utakuwa  umebarikwa  sana  usiache  kuomba  wala  kumtumikia  Bwana  katika  maisha  yako,barikiwa  sana  mtu  wa Mungu.

Ni mimi  ndugu  yako,
BARAKA  AUDAX
Injili  ya  Kristo  Zanzibar
0717  461006
Barikiwa  sana.





Comments

Popular Posts